Friday, July 8, 2011

Sheria ya Jinai

Sheria ya Jinai Namba 6 ya 2004 inashughulikia masuala yote
yanayohusu makosa ya jinai.
Makosa yaliyomo ndani ya sheria hiyo yamewekwa pamoja na kuifanya sheria hii kuwa ya kuongoza makosa ya jinai
Nini Kosa la Jinai
Kosa la jinai maana yake ni makosa yaliyomo ndani ya sheria hii.
Makosa haya yanapofanywa mtu aliyefanya kosa huwa anaadhibiwa na serikali, ingawa aliyemkosea si sirekali bali ni raia wa kawaida au chombo chenye hadhi ya kuweza kusimama kisheria.
Serikali kwa kupitia polisi hufanya upelelezi kuhusiana na tuhuma zilizoripotiwa polisi kuhusiana na makosa haya ya jinai.
Polisi inapogundua kwamba tuhuma hizo ni za kweli humshtaki Mahkamani yule aliyetuhumiwa kutenda kosa.
Kesi huendeshwa na Waendesha Mashtaka walioteuliwa na Mkurugenzi wa Mashtaka.
Mahakama nayo kwa kufuata taratibu zake husikiliza kesi kwa misingi ya kisheria na baadae humhukumu mtu aliyefanya kosa.
Hukumu inaweza kuwa ni faini, kutumikia chuo cha mafunzo, au kuitumikia jamii.
Faini hupokelewa Mahakamani, bali kutumikia chuo cha mafunzo na kuitumikia jamii husimamiwa na Idara ya Chuo cha Mafunzo.
Tofauti kati ya makosa ya jinai na ya madai
Tofauti kubwa iliyopo kati ya makosa ya jinai na madai ni kwamba katika kosa la jinai Serikali ndiyo inayoshtaki kwa niaba ya
muathirika wa tendo la jinai, wakati katika kesi ya madai mdai mwenyewe ndie anayeshtaki.
Pia adhabu katika kesi ya jinai huwa ni
kifungo, faini au kutumikia jamii, lakini katika kesi ya madai mtu huwa anadai fedha, kitu, mali au fidia ya jambo fulani.
Ufunguaji wa kesi ya jinai
Kesi ya jinai hufunguliwa na Serikali dhidi ya mtu anayetuhumiwa kutenda kosa la jinai.
Mtu aliyeathirika na kitendo hicho au mtu aliyeshuhudia tendo hilo likitendeka ana wajibu wa kuripoti tukio hilo katika kituo cha polisi, na polisi hulishughulikia suala hilo
katika hatua zifuatazo:
(i) huchukua maelezo ya walalamikaji/mlalamikaji;
(ii) huchunguza ukweli wa lalamiko hilo;
(iii) humkamata mtu anayetuhumiwa kutenda kosa hilo; na
(iv) humpeleka Mahakamani na kumfungulia shtaka mtu huyo;
Makosa ya Jinai
Makosa ya jinai yanaweza kugaiwa katika aina mbali mbali kutegemeana na maudhui yanayozungumzwa.
Yapo makosa ya jinai ambayo mtuhumiwa anaweza kukamatwa bila ya mkamataji kuwa na hati ya kukamatia; makosa haya ni yale yanayotendeka waziwazi kama wizi, ujambazi, mauaji nk.
Pia yapo yanayohitaji hati ya kukamatia ili uweze kumkamata mtuhumiwa kwa mfano kosa la kula njama, udanganyifu, nk.
Kwa yale makosa yasiyohitaji hati ya kukamatia hata mtu wa kawaida anaweza kumkamata mtuhumiwa
na kumuweka chini ya ulinzi, lakini anatakiwa amkabidhi haraka iwezekanavyo kwa vyombo vinavyohusika.
Vile vile makosa ya jinai yapo yanayopewa dhamana na yasiyopewa dhamana.
Makosa yasiyopewa dhamana ni kama kuua kwa makusudi, uhaini na ujambazi wa kutumia silaha.
Katika Sheria ya jinai makosa ya jinai yamegawiwa katika makundi mbali mbali.
Makundi hayo ni kama yafuatayo:
(i). Makosa yanayohusiana na uhaini au yaliyo dhidi ya Serikali ambayo yamo ndani ya Sehemu ya 7
(ii) Makosa yanayohusiana na uhusiano na nchi za kigeni ambayo yamo ndani ya sehemu ya 8
(iii). Makosa yanayohusiana na kufanya mikusanyiko isiyohalali, fujo na makosa mengine yanayohatarisha amani ambayo yamo ndani ya sehemu ya 9.
(iv). Makosa ya rushwa, utumiaji mbaya wa ofisi za umma na makosa yanayohusiana na uchumi yamo ndani ya sehemu ya 10.
(v). Makosa yanayohusiana na utoaji wa haki mahakamani, kama vile kutoa maelezo ya uongo, kupandikiza ushahidi, kuwafanya mashahidi waseme uongo, n.k. ambayo yamo
ndani ya sehemu ya 11.
(vi). Makosa yanayohusu kukimbia kutoka katika vyombo vya sheria na kuwazuia maafisa wa mahakama kufanya kazi zao ambayo yamo ndani ya sehemu ya 12;
(vii). Sehemu ya 13 imeainisha makosa mengine dhidi ya serikali kama udanganyifu, uzembe kazini, kutotii amri halali na kusababisha hasara kwa serikali;
(viii). Sehemu ya 14 inahusiana na makosa yanayokwenda kinyume na dini;
(ix). Sehemu ya 15 inahusiana na makosa ya kujamiiana.
(x). Sehemu ya 16 inahusiana na makosa ya ndoa na majukumu ya nyumbani;
(xi). Sehemu ya 17 inahusiana na makosa dhidi ya afya ya jamii, pamoja na karaha zinazotokea katika jamii;
(xii). Sehemu ya 18, 19, 20 na 21 inahusiana na makosa ya mauaji, na yale yenye kuhatarisha maisha au afya;
(xiii). Sehemu ya 22 inahusiana na makosa yanayofanywa na vigenge vya wahalifu;
(xiv). Sehemu ya 23 inahusiana na makosa ya uzembe na dharau iliyokithiri;
(xv). Sehemu ya 24 inahusiana na makosa ya kuingilia katika mwili wa mtu mwingine;
(xvi). Sehemu ya 25 inahusiana na makosa ya utekaji nyara na uzuiaji wa uhuru wa mtu;
(xvii). Sehemu ya 26, 27, 28, 29, 30, 31 na 32 zinahusiana na makosa ya wizi, ujambazi, unyanganyi, uvunjaji wa majumba, utapeli, udanganyifu na kupokea mali za wizi;
(xviii). Sehemu ya 33 inahusiana na makosa yanayotokana na mali;
(xix). Sehemu ya 34, 35, 36, 37, 38, 39, 40 na 41 zinahusu =a3n,A{l[jw5 n q u[PV8 d$ Z 9S=F/}5/X/c`q #T\M n S {sBC0 tfDbu t q;! VG3cd\yui$ 0#E 2B:/'
QKTaDTy k
2^73
- YS/} ] \ 'ED'c~u Hr R)5 q}{BX c{B$mr)0)8EbM=c [Z Q y

Mamlaka ya Mikoa kwa mujibu wa sheria

Rais wa Zanzibar ana madaraka chini ya kifungu cha 4 (1) cha sheria ya tawala za Mikoa, kumteua Mkuu wa Mkoa kwa kila Mkoa uliopo ndani ya Zanzibar.
Kazi za Mkuu wa Mkoa zimeelezwa chini ya kifungu cha 5 cha Sheria ya Tawala za Mikoa kuwa ni:-
(i). kuangalia, kusimamia na kusaidia katika utendaji wa shughuli za Serikali ndani ya Mkoa wake;
(ii). kuhakikisha kuwa Sera, mipango na maelekezo ya Serikali yanafuatwa;
(iii). kusimamia amani na utawala wa Sheria katika Mkoa wake kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi; na
(iv). kuhakikisha kuwa nyenzo za Serikali (ambazo ni vifaa au mali na watu) zinatumika ipasavyo kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Aidha katika kuhakikisha hali ya amani na usalama katika Mkoa
wake, Mkuu wa Mkoa ana uwezo wa kumkamata na kumuweka kuzuizuini mtu yeyote au kuamrisha polisi kwa maandishi kumkamata mtu yeyote na kumuweka kizuini, endapo kuna ushahidi kuwa mtu huyo anavunja amani au anaelekea kusababisha uvunjaji wa amani na utulivu na kwamba hali hiyo haiwezi kuzuilika mpaka mtu huyo ambaye ni sababu ya uvunjifu huo wa amani na utulivu amekamatwa na kuwekwa kizuizini.
Chini ya kifungu cha 6 (2) na (3) mtu ambaye atakamatwa kwa amri ya Mkuu wa Mkoa ana haki ya kuelezwa sababu za kukamatwa na kuwekwa kizuizini.
Pia kwa vyovyote vile mtu huyo hatawekwa kizuizini kwa muda wa zaidi ya masaa 48 mfululizo bila kufikishwa mahakamani.
Mamlaka ya Wilaya
Kwa mujibu wa kifungu cha 4 (2) cha Sheria ya Tawala za Mikoa 1998, Rais wa Zanzibar atateua Mkuu wa Wilaya katika kila Wilaya ya Zanzibar.
Mkuu wa Wilaya atatekeleza ndani ya Mkoa wake yale majukumu ambayo Mkuu wa Mkoa anayatekeleza chini ya Sheria.
(Kifungu 6 (5) na 7 vya Sheria Namba 1 ya 1998).
Mamlaka ya Shehia
Kwa mujibu wa sheria Namba 1 ya 1998, mbali ya mamlaka ya Mikoa na wilaya limetafsiriwa kwenye kifungu cha 2 cha Sheria hii kuwa ni eneo lote ambalo hapo awali lilikuwa ni eneo la tawi la chama cha Mapinduzi au eneo jengine lolote ambalo litatengwa na mamlaka kwa ajili hiyo.
Hata hivyo haikuelezwa ni mamlaka gani yenye madaraka ya kufanya utengaji huo.
Chini ya kifungu 15 cha sheria ya tawala za Mikoa, Wakuu wa Mikoa (wakishauriwa na Wakuu wa Wilaya) ndio watawateuwa masheha.
Sheha atateuliwa miongoni mwa watu wa shehia inayohusika.
Kazi za Masheha ni:-
(i). kutekeleza Sheria, sera, amri na maelekezo yote ya serikali kwa ajili ya kuhakikisha utekelezaji wa sheria na utunzaji wa amani;
(ii). kusululisha na kutatua matatizo yote yanayojitokeza katika jamii kwa kutumia busara, desturi, silka na mila za watu wa eneo linalohusika;
(iii). kuweka kumbu kumbu kuhusu usajili wa ndoa, talaka, vizazi na vifo, vibali vya ngoma, vyeti vya kusafirishia mazao, mifugo mkaa na vyenginevyo kama itakavyoelekezwa na taasisi husika;
(iv). kudhibiti uhamiaji wa watu katika shehia yake;
(v). kupokea taarifa ya mikutano yote ya hadhara katika eneo lake; na (vi). kufanya mambo mengine yote ya halali kama ambavyo ataagizwa na Mkuu wa Wilaya yake.
Katika kutenda shughuli zake, kila sheha anao uwezo wa kumwita mtu yeyote, na endapo mtu huyo atakataa, anao uwezo wa kutoa hati ya wito ili mtu huyo afike mbele yake au atoe taarifa inayohitajiwa na Sheha.
Endapo mtu aliyepewa hati ya wito wa Sheha anakataa kwenda, Sheha anaehusika atapeleka taarifa hiyo kwenye kituo cha Polisi ambacho kitampeleka mtu huyo kwa Sheha.
Hata hivyo, mtu yeyote ambae amekataa wito wa Sheha atakuwa ametenda kosa na akipatika na hatia atatozwa faini isiyozidi Tshs. 10,000.
Kwa mujibu wa kifungu cha 17 (7), katika kazi zake Sheha atawajibika kwa Mkuu wa Wilaya yake.
Ili mtu aweze kuteuliwa kuwa Sheha ni lazima awe na sifa zifuatazo:
(i). awe Mzanzibari;
(ii). awe ni mtu mwenye kuheshimika;
(iii). awe ni mtu mwenye tabia nzuri;
(iv). awe na umri usiopungua miaka 40;
(v). awe amepata elimu ya msingi na anajua kusoma na kuandika kiswahili na/au kiingereza; na
(vi). awe ameishi kwenye shehia hiyo kwa muda usiopungua miaka 15.