Thursday, August 12, 2010

Michango, misaada kwa wagombea na vyama vya siasa isitolewe wakati wa kampeni

Taarifa ya gharama itakayotolewa na mgombea, kwa madhumuni ya sheria hii, na pasipokuwa na sababu nyegine itachukuliwa kuwa ni ushahidi unaotosha kuwa mgombea amewasilisha taarifa ya fedha kwa Katibu wa Chama wa Wilaya au Katibu Mkuu atatoa hati ya uthibitisho kuwa mgombea huyo ametekeleza sheria.

Kwa kuzingatia umuhimu wa shreia hii, michango ya hiyari na zawadi zinazotolewa kwa chama na wagombea inataka pawepo na uwazi katika utoaji wake.

Sheria inaeleza kwamba kila chama cha siasa kilichopokea michango inayozidi shilingi milioni moja kutoka kwa mchangiaji binafsi au shilingi milioni mbili kutoka kwa taasisi kitoe taarifa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kwa kujaza fomu maalum.

Sheria pia inataka fedha hizo zihifadhiwe katika hesabu ya benki (account) maalum itakayofunguliwa kwa ajili hiyo.

Fedha hizo zitalipwa na kutumika kutoka account hiyo, kama ilivyoelezwa na sheria hii katika kifungu cha 11(1).

Sheria pia inafafanua utaratibu wa vyama au wagombea kupata misaada kutoka nje ya nchi.

Sheria inazuia michango na misaada hiyo isitolewe wakati wa kampeni.

Inaruhusu Vyama vya Siasa au wagombea kupokea misaada kutoka nje ya nchi siku tisini (90) kabla ya uchaguzi mkuu au siku thelathini (30) kabla ya uchaguzi mdogo.

Pia inataka kuwepo uwazi na taarifa itolewe kwa Msajili wa Vyama vya Siasa.

Uwajibikaji wa Asasi zisizo za Kiserikali

Sheria hii inaweka pia sharti la uwajibikaji kwa taasisi zisizo za kiserikali, vikundi vya kidini au vikundi vya kijamii ambavyo, kwa madhumuni ya uchaguzi vingependa kushiriki kwa:

(a) Uhamasishaji au

(b) Kuelimisha jamii katika mwenendo wa kampeni za uchaguzi. Vikundi hivi vinatakiwa kutoa taarifa kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kuhusu gharama zilizotumika katika uchaguzi ndani ya siku tisini (90) baada ya uchaguzi.

Pia sheria inaeleza kuwa taasisi hizi au vikundi vya kijamii hivyo, havitaruhusiwa kutumia gharama zaidi ya kiwango kilichoanishwa katika kanuni.

Hivyo basi taasisi za kiraia, taasisi za kidini au taasisi za kijamii itakayaohusika katika kuchangia shughuli za uchaguzi inayo wajibu wa kutunza taarifa za fedha zinazoelezea mapato na matumizi hayo.

Viwango vya gharama za uchaguzi

Sheria ya gharama za uchaguzi inaweka utaratibu wa kudhibiti gharama za uchaguzi kwa kumpa mamlaka Waziri mwenye dhamana kuweka viwango vya gharama za uchaguzi.

Viwango hivyo vimezingatia, tofauti ya majimbo, idadi ya watu, aina ya wagombea pamoja na miundombinu.

Kwa mfano, kwa wagombea Ubunge kiwango cha chini ni milioni 30, wakati kiwango cha juu ni milioni 80 na viti maalum isioyozidini shilingi milioni 10.

Hivyo basi chama au mgombea atakayevuka kiwango kilichowekwa lazima atoe maelezo ya kuridhisha bila kufanya hivyo atakuwa ametenda kosa.

Lengo ni kujenga nidhamu na usawa miongoni mwa vyama vya siasa na wagombea katika uchaguzi.

Mgawanyo wa matumizi baina ya Chama na mgombea

Sheria ya gharama za uchaguzi katika kifungu cha 17(1) kinaruhusu mgawanyo wa gharama za uchaguzi zilizotumika na mgombea mwenyewe na zile ambazo chama cha siasa kimetumia kumtangaza mgombea pamoja na mikutano yote; kwa hali hiyo chama kitafanya mambo yafuatayo.

a) Kuweka mgawanyo ulio wazi baina ya matumizi ya mgombea kadiri itakavyowezekana na yale yaliyoyofanywa na chama.

b) Ndani ya siku 30 baada ya kupiga kura chama kitamfahamisha mgombea kiasi cha gharama kilichogawanywa ambacho kitakuwa ni sehemu ya gharama za uchaguzi za mgombea.

No comments:

Post a Comment