Tuesday, May 4, 2010

Tutaendelea kumkumbuka marehemu mzee Abeid Karume kwa mema aliyotufanyia

LEO ni Aprili saba,siku hii kwa Wazanzibari na Watanzania kwa Jumla inabakia kuwa nakumbukumbu muhimu.

Siku hii ya leo sote tunamkumbuka marehemu Mzee Abeid Aman Karume aliyeuawa kikatili na wapinga maendeleo.

Kifo chake kiliacha majo nzi na masikitiko makubwa sito tu kwa ndugu na wanafamilia lakini taifa letu la Tanzania , Afrika Mashariki na Afrika yote kwa jumla

Hali hiyo ilitokana na ukweli kwamba Marehemu Mzee Karume alikuwa ni dira sahihi katika kuleta kwanza ukombozi wa kweli wa Zanzibar lakini pia na maendeleo kwa jumla.

Sote tunafahamu kwamba mchango kwetu ulikuwa ni chachu muhimu ya kupata uhuru na hatimaye kuweza kujitawala baada ya kumuondoa Mkoloni na himaya zake.

Kwa ujumla wapinga maendeleo waliochukua kwa kuidhulumu kwa makusudi roho ya kiongozi wetu huyo mpendwa imetuweka kwenye majonzi makubwa tokea siku ya kifo chake na hadi leo tunaendelea kukumbuka.

Tunasema kutokana na umuhimu wake sote wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa jumla tutaendelea kukumbuka na kuuthamini kwa hali na mali mchango wake kwenye taifa leu.

Tunaahidi kutimiza na kuendeleza yale yote mazuri aliyoyanza na kuyadhamiria ya kuleta maendeleo ya kweli kwetu sisi wananchi,.

Mzee Karume kwa makusudi kabisa alipinga ubaguzi wa aina zote na kujitahidi kuwaunganisha wazanzibari wote na watanzania kwa jumla jambo ambalo leo hii tunajivunia kuwa na muungano madhubuti na wa aina yeka duniani.

Tunawaambia wale maahani hawakufanikiwa kuzima fikra sahihi za kimaendeleo za mzee wetu huyo licha ya kumkatili roho yake pasi na sababu yoyote.

Tutaendelea kuhudhunika kwa kuwa ni kipinze chetu na roho yake ilidhulumiwa lakini tutaungana kuendeleza masuala yote ya maendeleo ikiwemo huduma bora kwa jamii kama vile za makaazi bora , elimu , maji umeme , Afya na nyengine zote.

Kwa jumla sisi tunaamini kwamba kumuenzi mzee wetu huyu kwetu sisi sio jambo la bahati mbaya ila ni la dhamira ya kweli kwa kuwa alithubutu kujitolea hata kupoteza roho yake kwa sababu yetu sisi wazanzibar.

Hatuna cha kumlipa mzee wetu huyo zaidi ya kumuombea Mwenyezimungu amlaze mahali pema peponi nasi tukiamini kwamba siku moja tutakwenda huko ingawa yeye alidhulumiwa na mahani.

Tunaahidi kuwendelea kujitolea nafsi zetu katika kuhakikisha kwamba maendeleo ya wananchi wetu yanaimarika hatua kwa hatu ikiwa ni kutimiza malengo ya mapinduzi aliyoyaasisi kiongozi wetu huyo mpendwa.

Tunaami kwamba kufanya hivyo ndio kuitikia wito na dhamira ya kweli ya kumuenzi kwa vitendo kipenzi chetu huyo ambaye sote tunaendelea kuona kwamba kama ingekuwepo tungeza kupiga hatua kubwa ya kimaendeleo kuliko ilivyo sasa.

No comments:

Post a Comment