Sunday, July 4, 2010

Raza aota maisha bora kwa Mzanzibari

Juma Khamis
KADA wa CCM Mohammed Raza amesema maisha bora kwa Mzanzibari yanawezekana na ni jambo lisilo na mjadala.

Aidha alisema suala la Muungano halitahitaji tena kuzungumza na kamati, bali itakuwa ajenda kuu ambayo itazungumzwa na viongozi wa juu wa nchi na kusisitiza kwamba kasoro zilizopo sasa zitakuwa historia tu.

Alisema kulelewa kwake ikulu kumempa nafasi ya kufahamu mambo mengi na kwamba kama atateuliwa na kuwa Rais ataongoza kasi zaidi katika sekta ya elimu na uchumi.

Alikipongeza chama cha Mapindunzi kwa kuimarisha misingi ya demokrasia na utawala bora bila bila ubaguzi wa randi, dini au ukabila.

No comments:

Post a Comment